watu 5 wamefariki dunia kutokana na shambulizi la bomu.
Shambulizi la bomu katika uwanja wa soka Kusini mwa Somalia, limesababisha
vifo vya watu watano na wengine 12 kujeruhiwa.,ambapo hii ni mara ya kwanza kwa
shambulizi la kigaidi kulenga uwanja wa michezo nchini humo.
RAIS WA SOMALIA ABDULLAH MOHAMED. |
Maafisa wanasema shambulizi hilo lilitokea katika mji wa Barawe
jimboni Shabelle, wakati watu wakitazama mpira wa soka.
Polisi wanalishuku kundi la kigaidi la Al Shabab kuhusika katika
shambulizi hilo ambalo limesababisha vifo hivyo pamoja na majeruhi.
Rais wa Somalia Bw Abdullahi Mohamed amesema adui pekee wa nchi
hiyo ni Al Shabab.
watu 5 wamefariki dunia kutokana na shambulizi la bomu.
Reviewed by safina radio
on
April 13, 2018
Rating:
No comments