KANSELA MERKEL ASEMA SERIKALI YAKE IKO TAYARI


Kansela Angela Merkel amesema kuwa serikali yake iko tayari kuiongoza Ujerumani, licha ya kuwepo na hali ya kurushiana maneno miongoni mwa viongozi wa vyama vinavyounda serikali yake.
Image result for PICHA YA MERKEL


Akizungumza baada ya mkutano wa siku mbili na baraza lake la mawaziri, Merkel amesema huenda kukawa na majibizano miongoni mwa viongozi, lakini ni wazi kuwa ipo nia ya kufikia makubaliano kuhusu masuala ya nchi.

 Merkel alianza muhula wake wa nne, na ambao unaonekana kuwa wa mwisho, akikabiliwa na changamoto ya kuongoza serikali ya muungano kati ya kundi la vyama vyake vya kihafidhina vya CDU na CSU, na chama sha SPD wakati umaarufu wake ukiendelea kupungua kufuatia mgogoro wa wakimbizi ulioanza mwaka wa 2015 nchini Ujerumani.  

KANSELA MERKEL ASEMA SERIKALI YAKE IKO TAYARI KANSELA MERKEL ASEMA SERIKALI YAKE IKO TAYARI Reviewed by safina radio on April 12, 2018 Rating: 5

No comments