WANAFUNZI WA VYUO WAMETAKIWA KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA
Wanafunzi wa vyuo mbalimbali hapa nchini wametakiwa
kuwa na utaratibu wa kujiunga na bima ya afya pamoja na mali zao ili kuweka
akiba pindi wanapokumbwa na majanga mbalimbali ili wafidiwe kwa kile
walichokiekeza.
Hayo yamesemwa jijini Arusha na Meneja wa
Kanda ya Kaskazini wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Nchini TIRA Elieza Rekiza wakati
akitoa elimu ya matumizi ya bima kwa
wanafunzi wa Chuo cha Ufundi Stadi VETA kilichopo Oljoro mkoani Arusha.
Aidha, amesema kuwa bado kuna tatizo kubwa la
uelewa mdogo kwa wananchi kuhusu umuhimu wa bima hizo hivyo ni vyema elimu ikatolewa
mara kwa mara ili wananchi wapate uelewa mkubwa zaidi juu ya suala hilo.
Kwa upande wake, Meneja wa kanda ya kaskazini
wa Kampuni ya Zanzibar Insuarrence Cooporation Bw Mohamed Matumla amesema kuwa
makundi ya vijana yaliyoko katika taasisi za elimu wanahitaji kuelimishwa na
kuwa watumiaji wakubwa wa huduma ya bima.
Hata hivyo baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho
cha ufundi VETA Oljoro wamesema kuwa mafunzo ya uelewa juu ya huduma za bima
inasaidia kujua kiundani kuhusu shughuli za bima na namna zinavyoweza
kuwasaidia.
WANAFUNZI WA VYUO WAMETAKIWA KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA
Reviewed by safina radio
on
April 17, 2018
Rating:
No comments