MFALME WA SWAZILAND MSWATI WA TATU AMETANGAZA KUBADILISHA JINA LA NCHI HIYO.
Mfalme wa Swaziland, Mswati wa Tatu, ametangza kubadilisha jina
la nchi yake ambayo sasa itajulikana kama Ufalme wa ESwatini.
MFALME MSWATI WA TATU |
Rais huyo ametangaza uamuzi huo wa ghafla katika sherehe za
mwaka wa 50 wa uhuru wa Uswazi pamoja na maadhimisho ya siku ya kuzaliwa kwake
ambapo pia ametimiza miaka 50.
Katika mikutano kadhaa ya hadhara Mfalme Mswati wa Tatu amekuwa
akiitaja nchi yake kwa jina la eSwatini, kwa maana ya 'ardhi au nchi ya
Waswazi' kwa lugha ya Kiswati au Kiswazi.
Mfalme Mswati amesema mabadiliko hayo yatasababisha nchi yake
irejee katika jina lake la asili kabla ya zama za ukoloni wa
Muingereza,ambapo Nchi hiyo ndogo ya kusini mwa Afrika ilipata uhuru wake mwaka
1968.
Aidha mfalme huyo amesema jina hilo jipya pia litasaidia
kutatuliwa kwa tatizo la kimataifa ambapo watu wengi wamekuwa wakiitaja nchi
hiyo kuwa ni Switzerland, nchi ya Ulaya Magharibi.
MFALME WA SWAZILAND MSWATI WA TATU AMETANGAZA KUBADILISHA JINA LA NCHI HIYO.
Reviewed by safina radio
on
April 20, 2018
Rating:
No comments