WACHUNGUZI KUZURU DOUMA HUKO SYRIA.


Urusi imesema kuwa wachunguzi wa silaha za kemikali nchini Syria wataruhusiwa kuzuru katika eneo linalodaiwa kushambuliwa na silaha za sumu siku ya Jumatano
Kundi hilo la kimataifa limekuwa nchini humo tangu siku ya Jumamosi lakini halijaruhusiwa kuingia Douma.

Image result for PICHA YA ENEO LILILOSHAMBULIWA NCHINI SYRIA


Shambulio hilo la siku ya Aprili 7 lilifuatia shambulio linguine dhidi ya serikali ya Syria lililotekelezwa kwa pamoja na Marekani, Uingereza na Ufaransa wiki moja baadaye.

Syria na mshirika wake Urusi wamekana shambulio lolote la kemikali huku Urusi ikitaja madai hayo kama 'yaliopangwa'.

Mapema siku ya Jumanne , chombo cha habari cha Syria kilisema kuwa ulinzi wa angani wa taifa hilo ulikabiliana na shambulio la makombora juu ya anga ya magharibi mwa mji wa Homs.












WACHUNGUZI KUZURU DOUMA HUKO SYRIA. WACHUNGUZI KUZURU DOUMA HUKO SYRIA. Reviewed by safina radio on April 17, 2018 Rating: 5

No comments