MAGUFULI AWAACHIA HURU ZAIDI YA WAFUNGWA 3000.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk. John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa wote kupunguziwa robo ya adhabu zao baada ya punguzo la kawaida la moja ya tatu ambapo wafungwa hao sharti wawe wametumikia robo ya adhabu zao gerezani isipokuwa wafungwa walioorodheshwa kwenye ibara ya pili.

Image result for magufuli

Wafungwa wengine waliopatiwa msamaha huo ni wale wagonjwa wenye magonjwa ya kifua kikuu, UKIMWI na Saratani ambao wako kwenye Hatua ya mwisho (terminal stage).

Pia, wengine waliopata msamaha huo ni wafungwa wazee wenye umri wa miaka sabini au zaidi, wafungwa wa kike walioingia gerezani wakiwa na ujauzito, pamoja na walioingia gerezani na watoto wanaonyonya na wasio nyonya.

Aidha wafungwa wenye ulemavu wa akili wametakiwa kuthibitishwa na jopo la waganga chini ya Mwenyekiti ambaye ni Mganga Mkuu wa Mkoa au Mganga Mkuu wa Wilaya.

Hata hivyo, Msamaha huo hautawahusisha wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa au kwa makosa ya kujaribu kuwaua wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kunyongwa na adhabu hiyo kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au kifungo gerezani, wafungwa wanaotumikia kifungo gerezani, wafungwa wanaotuhumiwa na makosa ya kujihusisha na usafirishaji na matumizi ya dawa za kulevya kama vile Cocain, Heroin na Bangi.

Wafungwa elfu tatu mia tatu kumi na tisa watafaidika na msamaha huo ambapo mia tano themanini na tano wanaachiliwa huru leo, huku wafungwa   elfu  mbili  mia saba  thelathini  na  nne watabaki gerezani kumalizia sehemu ya kifungo kilichobaki baada ya msamaha huo.

Mategemeo ya serikali ni kuwa wafungwa hao watarejea katika jamii na kushirikiana na wanajamii katika ujenzi wa taifa na  watajiepusha na kutenda makosa ili wasirejee gerezani.

MAGUFULI AWAACHIA HURU ZAIDI YA WAFUNGWA 3000. MAGUFULI AWAACHIA HURU ZAIDI YA WAFUNGWA 3000. Reviewed by safina radio on April 26, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.