WATU 18 WAMEFARIKI NCHINI RWANDA KUTOKANA NA MVUA ZINAZOENDELEA.
Mvua
kubwa imeendelea kunyesha katika nchi za Afrika Mashariki na Kati,ambapo Nchini
Rwanda watu kumi na wanane wamepoteza maisha wiki hii, baada ya kusombwa na
maji.
Mbali
na maaafa hayo, makaazi ya watu yameharibika hasa wale wanaoishi katika maeneo
ya milima.
Nchini
Kenya, hali imekuwa vivyo hivyo baada ya mvua kubwa inayoendelea kunyesha kusababisha
madhara makubwa, ikiwa ni pamoja na baadhi ya mitaa ya jiji kuu Nairobi kama
Buruburu kujaa maji.
Nchini
Burundi, hasa katika mji mkuu wa nchi hiyo Bujumbura, maeneo ya Maramvya,
Carama na maeneo ya mabondeni ndio yameathrika zaidi na mvua hizo zinazoendelea
kunyesha.
WATU 18 WAMEFARIKI NCHINI RWANDA KUTOKANA NA MVUA ZINAZOENDELEA.
Reviewed by safina radio
on
April 25, 2018
Rating:
No comments