MKUU WA MKOA WA GEITA MHANDISI ROBERT GABRIEL AZITAKA HALMASHAURI ZA MKOA HUO KUSIMAMIA NA KUWATAMBUA WACHIMBAJI WADOGO.
Mkuu wa Mkoa wa
Geita Mhandisi Robart Gabriel amezitaka halmashauri za Mkoa huo kusimamia na
kuwatambua wachimbaji wadogo wa madini wote walioko kwenye Halmashauri zao.
Akizungumza katika
kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Geita Mhandisi Gabriel
amesema kuwa wachimbaji wengi bado hawatambuliki serikalini, hivyo kushindwa
kupata kodi stahiki kutoka kwa wachimbaji hao.
Akizungumza kwa
niaba ya madiwani wa halmashauri hiyo ya Geita Diwani Jeremiah Ikangala amesema
kuwa tatizo la kutokusanywa kwa mapato katika eneo la madini wamelibaini na
tayari wamelichukulia hatua suala hilo.
Aidha baadhi ya
watu waliokuwepo katika Mkutano huo wameunga mkono tamko la Mkuu wa mkoa huyo na
kusema kuwa jitihada kubwa zinastahili kuwekwa katika usimamizi wa shughuli za
uchimbaji wa madini kwa kuwa kuna mapato mengi yanayotakiwa kulipwa serikalini.
MKUU WA MKOA WA GEITA MHANDISI ROBERT GABRIEL AZITAKA HALMASHAURI ZA MKOA HUO KUSIMAMIA NA KUWATAMBUA WACHIMBAJI WADOGO.
Reviewed by safina radio
on
April 26, 2018
Rating:
No comments