MAWAZIRI WA ELIMU AFRIKA WATAKUTANA KUJADILI MAENDELEO ENDELEVU KUHUSU ELIMU KWA BARA LA AFRIKA.
Mawaziri
wa elimu kutoka nchi za Afrika wiki ijayo watafanya mkutano wa siku tatu mjini
Nairobi, nchini Kenya ili kutathmini hadhi ya Malengo ya Maendeleo Endelevu
kuhusu elimu katika bara hilo.
Mkutano
huo ulioandaliwa na Shirika la Elimu na Sayansi la Umoja wa Mataifa (UNESCO) pamoja
na Umoja wa Afrika, utawakutanisha mawaziri wa elimu kutoka Afrika, watunga
sera na washauri kutoka sekta ya umma na binafsi kuhusu suala la elimu.

UNESCO imesema wajumbe pia watajadili,
kuongeza uelewa na kubadilishiana maoni kuhusu jinsi ya kuunganisha Malengo
Endelevu ya Maendeleo na Mkakati wa Elimu kwa bara la Afrika katika kuboresha
mifumo ya ajenda, sheria ya elimu, sera, mipango, ufadhili, usimamizi na
mawasiliano.
MAWAZIRI WA ELIMU AFRIKA WATAKUTANA KUJADILI MAENDELEO ENDELEVU KUHUSU ELIMU KWA BARA LA AFRIKA.
Reviewed by safina radio
on
April 18, 2018
Rating:
No comments