ILI KUKABILIANA NA WIZI WA KIMTANDAO SERIKALI YAJIWEKEA MIKAKATI MBALIMBALI.


Naibu waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Mh Atashasta Nditiye amesema kuwa ili kukabilina na wizi wa kimtandao hapa nchini serikali imejiwekea mikakati mbalimbali ikiwemo kuwatumia wataalamu wake wa ndani wa TEHAMA ili kujadiliana namna ya kumaliza wizi huo.

Image result for PICHA YA TEHAMA


Mh Nditiye ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Busekelo Mh Wilfred Mwakibete aliyetaka kujua serikali imejiwekea mikakati gani ili kupambana na wizi wa kimtandao unaoendelea hapa nchini.

Amesema kuwa ni kweli wizi wa kimtandao unaendelea hapa nchini na kwa kutambua hilo serikali itakaa na wataalamu wa TEHAMA ili kutengeneza progmu maalumu itakayosaidia kuzuia uhalifu wa kimtandao.

Ameongeza kuwa mbali na serikali kukutana na wataalamu hao imepanga pia kwenda kujifunza kwa nchi ambazo zimefanikiwa kupambana na uhalifu wa kimtandao ikiwemo nchi za Israel,India na Marekani ili kujua ni njia gani walizotumia kupambana na uhalifu huo.

Bunge la bajeti linaendelea mjini Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti ya wizara ya ujenzi uchukuzi na mawasiliano kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019 iliyowasilishwa hapo jan na waziri wa wizara hiyo Mh Makame Mbarawa.

ILI KUKABILIANA NA WIZI WA KIMTANDAO SERIKALI YAJIWEKEA MIKAKATI MBALIMBALI. ILI KUKABILIANA NA WIZI WA KIMTANDAO SERIKALI YAJIWEKEA MIKAKATI MBALIMBALI. Reviewed by safina radio on April 24, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.