SERIKALI INA MPANGO WA KUIMARISHA MINARA YA SIMU ILIYOKO MIPAKANI.


Naibu waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Mh Atashanta Nditiye amesema kuwa serikali ina mpango wa kuimarisha minara ya simu iliyopo mipakani ili kuzuia mwingiliano wa mawasiliano kati ya nchi na nchi.

Image result for PICHA YA MNARA WA SIMU

Mh Nditiye ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Vunjo Mh James Mbatia aliyetaka kujua serikali ina mpango gani wa kuzuia mwingiliano wa mawasiliano ya simu kwa wananchi walioko katika maeneo ya Vunjo na Rombo mkoani Kilimanjaro.

Amesema kuwa maeneo mengi yaliyoko mipakani hapa nchini yanakabiliwa na mwingiliano wa mawasiliano ya simu kutoka nchi jirani na ili kukabiliana na changamoto hiyo serikali kupitia mfuko wa fursa kwa wote wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA itaimarisha minara iliyoko katika mipaka hiyo ili kumaliza tatizo hilo.

Hata hivyo bunge la 11 mkutano wa 11 linaendelea Jijini Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2018/219.





SERIKALI INA MPANGO WA KUIMARISHA MINARA YA SIMU ILIYOKO MIPAKANI. SERIKALI INA MPANGO WA KUIMARISHA MINARA YA SIMU ILIYOKO MIPAKANI. Reviewed by safina radio on April 27, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.