JMEC YASEMA KUWA TAREHE MPYA YA MAZUNGUMZO YA AMANI SUDANI KUSINI ITATANGAZWA NA MWENYEKITI WA IGAD.


Wafuatiliaji wa amani nchini Sudan Kusini wamesema kuwa mazungumzo yajayo ya amani yaliyopangwa kufanyika tarehe 26 Aprili mwaka huu yameahirishwa hadi taarifa itakapotolewa.
Image result for sudani kusini
Tume ya Ufuatiliaji na Tathmini JMEC imesema kuwa tarehe mpya ya mazungumzo hayo itatangazwa na mwenyekiti wa baraza la mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali ya Nchi za Afrika Mashariki IGAD.

Hata hivyo kwa mujibu wa habari zilizotolewa ,Tume hiyo inasema kuwa kuahirishwa kwa kwa mazungumzo hayo kutatoa nafasi ya mazungumzo yenye ufanisi kwa wadau mbalimbali wanaohusika na masuala hayo ya amani.

JMEC YASEMA KUWA TAREHE MPYA YA MAZUNGUMZO YA AMANI SUDANI KUSINI ITATANGAZWA NA MWENYEKITI WA IGAD. JMEC YASEMA KUWA TAREHE MPYA YA MAZUNGUMZO YA AMANI SUDANI KUSINI ITATANGAZWA NA MWENYEKITI WA IGAD. Reviewed by safina radio on April 18, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.