SHIRIKA LA NDEGE LA ETHIOPIA KUENEZA SHUGHULI ZAKE NCHINI CHINA.


Shirika la Ndege la Ethiopia limesema lina nia ya kueneza soko lake nchini China na kuwa shirika la ndege la kirafiki kati ya China na Afrika.

Image result for PICHA YA NDEGE YA SHIRIKA LA NDEGE LA ETHIOPIA

Hayo yamesemwa kwenye ripoti ya Shirika hilo iliyowasilishwa kwenye bunge la nchi hiyo, ambayo pia imesema zaidi ya raia 4,000 wa China wanapanda ndege yao kila siku.

Mkuu wa ofisi ya huduma za kimataifa ya Shirika hilo Bw. Esayas Woldemariam amasema Shirika hilo limechukua hatua kadhaa ili kuwavutia wageni wa China, ikiwemo kituo cha kuuliza maswali kwa Kichina na wahudumu wa China wanaotoa huduma ya chakula cha kichina.

SHIRIKA LA NDEGE LA ETHIOPIA KUENEZA SHUGHULI ZAKE NCHINI CHINA. SHIRIKA LA NDEGE LA ETHIOPIA KUENEZA SHUGHULI ZAKE NCHINI CHINA. Reviewed by safina radio on April 19, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.