UTOAJI WA MAFUNZO CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI KUSAIDIA KUFUTA UPOTOSHAJI.


Wanahabari Mkoani Njombe wamesema kuwa utoaji wa mafunzo ya chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi kwa watoto wa umri wa miaka 14 utasaidia kufuta upotoshaji wa lengo la utoaji wa chanjo hiyo kwa jamii.

Image result for PICHA YA WANAHABARI MKOANI NJOMBE
WANAHABARI WA MKOA WA NJOMBE
Wakizungunza mara baada ya kupatiwa mafunzo hayo baadhi ya wamahabari wamesema kuwa mafunzo hayo yatasaidia wanahabari kusahihisha mitazamo tofauti iliyopo kwenye jamii na lengo la chanjo hali inayosababisha watoto wengine kukosa chanjo hiyo.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dk. Buni Mwamasage amewataka wanahabari hao kufuata weledi wao kutoa elimu ya kutosha kwa jamii ili kufanikisha azma ya serikali ya kuzuia maambukizi ya saratani ya kizazi kwa miaka ya baadae.

Aidha, amesema kuwa kutokana na utafiti wa kisayansi kumebainika kuwa umri wa miaka 14 ni mzuri katika kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo kwa kuwa wasichana katika umri huo hawajajihusisha na tendo la ndoa huku akibainisha kuwa huduma ya chanjo hiyo itatolewa katika vituo vya serikali na vituo vya mashirika ya kijamii.

Saratani ya Mlango wa Kizazi imekuwa tishio kwa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania ambapo takwimu zinaonesha kuwa takribani watu elfu hamsini hupoteza maisha kila mwaka hapa nchi kutokana na ugonjwa huo.

UTOAJI WA MAFUNZO CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI KUSAIDIA KUFUTA UPOTOSHAJI. UTOAJI WA MAFUNZO CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI KUSAIDIA KUFUTA UPOTOSHAJI. Reviewed by safina radio on April 23, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.