IMEBAINISHWA KUWA MANENO MABAYA YANAWEZA KUHARIBU MFUMO WA MAISHA.
Imebainishwa kuwa kuna uwezekano
mkubwa wa maneno mabaya yanayotamkwa juu ya mtu kupata uhalali na yakaharibu kabisa
mfumo mzima wa maisha ya mtu huyo.
Huduma ya redio safina
kesho katika ukumbi wa maombi uliopo Mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili
asubuhi hadi saa sita mchana imekuandalia maombi maalumu ya kufuta maneno mabaya
yaliyotamkwa juu watu ili wasifanikiwe katika maisha yao.
Aidha, maneno mabaya yaliyotamkwa
juu ya baadhi ya watu yamekuwa mkosi
kwani husababisha kukosa kazi,wengine kushindwa kumalizia ujenzi wa nyumba, huku
wengine wakishindwa kusoma kutokana na magonjwa ya mara kwa mara pamoja na
kukosa ada ya masomo.
Vile vile, kutokana na maneno
mabaya yaliyotamkwa juu ya maisha yao kupata kibali yamesababisha watu kushindwa
kuoa na kuolewa, kupata watoto katika ndoa zao, kuvunjika kwa mahusiano ya
urafiki au uchumba hadi kusababisha migogoro katika jamii na Taifa kwa ujumla.
Hata hivyo, mtu atatatakiwa
kufika kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda na kielelezo cha kitendo cha
kiimani cha mzao wa mzabibu [Damu ya Yesu] kwa ajili ya kufanya kitendo cha kiimani
cha kufuta maneno yote mabaya ambayo yametamkwa na adui juu ya maisha ya watu
ili wasiweze kufanikiwa.
IMEBAINISHWA KUWA MANENO MABAYA YANAWEZA KUHARIBU MFUMO WA MAISHA.
Reviewed by safina radio
on
March 28, 2018
Rating:
No comments