NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI MH. ABDALAH AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA


Naibu waziri wa mifugo na uvuvi Mh Abdalah Ulega ameipongeza halmashauri ya wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma kwa kuweka mikakati dhabiti ya kupambana na uvuvi haramu.

Image result for PICHA YA NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI MH ABDALLAH ULEGA
Naibu waziri wa mifugo na uvuvi Mh Abdalah Ulega 

Mh Ulega ametoa pongezi hizo alipokuwa katika ziara ya kukagua mwalo wa Miyobozi uliko wilayani Uvinza mkoani humo ambapo amesema kuwa jitihada hizo za wilaya zitasaidia kwa kiasi kikubwa katika kuongeza mapato ya halmashauri na serikali.

Aidha naibu waziri huyo amesisitiza suala la mapambano dhidi ya uvuvi haramu na ulinzi wa rasilimali za uvuvi ambapo amewaagiza wakazi wa wilaya ya Uvinza kuacha utamaduni wa kuagiza samaki kutoka nje ya nchi.

Ameongeza kuwa fedha nyingi zimeekezwa katika mwalo wa Miyobozi na kutaka wavuvi katika eneo hilo kutumia vizuri mwalo huo ambao una hadhi ya kimataifa kwani  kwa mwaka wa fedha uliopita mwalo huo ulichangia kiasi cha shilingi milioni 28.

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI MH. ABDALAH AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI MH. ABDALAH AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA Reviewed by safina radio on March 19, 2018 Rating: 5

No comments