SHUGHULI ZA KIBINADAMU KATIKA VYANZO VYA MAJI YAPELEKEA VYANZO HIVYO KUPOTEZA UWEZO WA KUZALISHA MAJI NA KUHATARISHA USALAMA WA MAJI.


Imeelezwa kuwa uhifadhi wa mazingira katika  nyanzo vya maji bado ni changamoto  kubwa  katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati Mkoani Manyara  jambo ambalo linapelekea vyanzo vya maji kupoteza  uwezo wa kuzilisha maji na kuhatarisha  usalama wa maji.

Image result for Mkuu wa Wilaya ya Babati Raymond
Mkuu wa Wilaya ya Babati Raymond Mushi.
 Akisoma Taarifa ya hiyo mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Babati Raymond Mushi  wakati  wa  maadhimisho ya wiki ya Maji  iliyofanyika katika Kijiji cha Seloto Kata ya Dareda  Mhandisi wa maji wa Halmahauri hiyo Bw Samweli Tluway  amesema kumekuwa na shughuli nyingi za kibinadamu  katika vyanzo vya maji.

Amesema kuwa uchafuzi na uharibifu wa vyanzo vya maji  unasababishwa  na shughuli za kilimo  zinazofanyika  kwenye vyanzo vya maji, uchungaji wa mifugo,ujenzi wa makazi  ya kuishi, ujenzi wa vyoo pamoja na ukataji miti na utengenezaji wa mkaa ndani ya vyanzo vya maji.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya hiyo Raymond Mushi amesema kuwa ni jukumu la kila mwananchi kutunza vyanzo vya maji na kupanda miti  maeneo yanayozunguka  vyanzo vya maji  na kutokufanya shughuliz zinazoweza kuathiri  vyanzo vya maji hususani kilimo  na ufugaji.

Amesema kuwa hali ya maji inaridhisha lakini haijafikia kiwango kinachotakiwa  hivyo watu  wote kwa ujumla wanapaswa kutambua umuhimu wa maji katika maisha yao  hivyo ni muhimu kushirikiana kutunza vyanzo hivyo ili viwasaidie.






SHUGHULI ZA KIBINADAMU KATIKA VYANZO VYA MAJI YAPELEKEA VYANZO HIVYO KUPOTEZA UWEZO WA KUZALISHA MAJI NA KUHATARISHA USALAMA WA MAJI. SHUGHULI ZA KIBINADAMU KATIKA VYANZO VYA MAJI YAPELEKEA VYANZO HIVYO KUPOTEZA UWEZO WA KUZALISHA MAJI NA KUHATARISHA USALAMA WA MAJI. Reviewed by safina radio on March 23, 2018 Rating: 5

No comments