WAKAZI WAYAKIMBIA MAKAZI YAO, GHOUTA MASHARIKI KARIBU NA MJI MKUU WA SYRIA, DAMASCUS.


Maelfu ya raia wameukimbia mji wa Ghouta Mashariki nchini Syria baada ya mwezi mzima wa mfulululizo wa mashambulizi ya vikosi vya Serikali ambavyo vinakaribia kuudhibiti kabisa mji huo kutoka kwa waasi nje kidogo ya jiji la Damascus.
Image result for Ghouta Mashariki
Baadhi ya waokoajia na watu wakizidi kukimbia kutokana na mashambulizi yanayoendelea.
Rais wa Bashar al-Assad ameendelea kujiimarisha madarakani wakati huu vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo vikiingia mwaka wa nane.
Assad ameendelea kusisitiza kuwa mashambulizi hayo yataendelea hadi pale ngome hiyo ya upinzani inayosalia itakapoangushwa huku vikosi vyake vikiwa vimefanikiwa pakubwa katika vita vya kuuchukua mji wa Ghouta ambao wakati fulani ulikuwa ngome kuu ya wapiganaji waasi.
Waangalizi wa masuala ya vita wanasema kuwa kwa sasa vikosi vya Syria vimefanikiwa kushikilia asilimia 70 ya mji huo na kuwagawa wapiganaji waasi katika makundi matatu ambayo hayana uwezo tena wa kukabiliana na vikosi vya Serikali na washirika wake nchi ya Urusi.
Waangalizi wa haki za binadamu wanasema idadi ya raia waliokimbia ndani ya siku moja kutoka kwenye mji huo ni kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa katika historia ya vita vya Syria.


WAKAZI WAYAKIMBIA MAKAZI YAO, GHOUTA MASHARIKI KARIBU NA MJI MKUU WA SYRIA, DAMASCUS. WAKAZI WAYAKIMBIA MAKAZI YAO, GHOUTA MASHARIKI KARIBU NA MJI MKUU WA SYRIA, DAMASCUS. Reviewed by safina radio on March 16, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.