TRUMP, , AMTEUA LARRY KUDLOW, MCHAMBUZI WA MASUALA YA FEDHA KUWA MSHAURI MPYA WA MASUALA YA UCHUMI KATIKA IKULU YA WHITE HOUSE.


WASHINGTON.

Rais Donald Trump wa Marekani amemteuwa Mchambuzi wa masuala ya fedha katika televisheni nchini Marekani, Larry Kudlow kuwa mshauri mkuu mpya wa masuala ya uchumi katika Ikulu ya Marekani ya White house.
Image result for Rais Donald Trump
Rais Donald Trump.

Kudlow amelieleza shirika la habari la AP kuwa amekubaliana na uteuzi huo wa rais Donald Trump kuhudumu kama mshauri wa masuala ya uchumi.
Kudlow atachukua nafasi ya Gary Cohn ambaye alitangaza wiki iliyopita kuwa atajiuzulu nafasi hiyo baada ya kupinga mipango ya rais Donald Trump inayohusiana na viwango vipya vya kodi kibiashara.

Kudlow mwenye umri wa miaka 70 ni mchambuzi mwandamizi katika kituo cha Televisheni cha CNBC.







TRUMP, , AMTEUA LARRY KUDLOW, MCHAMBUZI WA MASUALA YA FEDHA KUWA MSHAURI MPYA WA MASUALA YA UCHUMI KATIKA IKULU YA WHITE HOUSE. TRUMP, , AMTEUA LARRY KUDLOW, MCHAMBUZI WA MASUALA YA FEDHA KUWA MSHAURI MPYA WA MASUALA YA UCHUMI KATIKA IKULU YA WHITE HOUSE. Reviewed by safina radio on March 15, 2018 Rating: 5

No comments