TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA ISRAEL ILI KUIMARISHA JESHI LA ULINZI
Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Dr Hussen
Mwinyi amesema kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na serikali ya Israel katika
kuimarisha jeshi la ulinzi la wananchi Tanzanaia JWTZ ili liweze kukabiliana na vitendo vya
kiuhalifu na ulinzi wa amani.
Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Dr Hussen Mwinyi |
Dr Mwinyi ameyasema hayo leo jijini Dar-es-salaam
wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ziara ya siku tatu hapa nchini
ya waziri wa ulinzi wa Israel Azegdo Lebaman,ambapo amesema kuwa JWTZ imekuwa
na ushirikiano na Israel ambayo inasaidia mafunzo mbalimbali ya kijeshi kwa
maafisa wa jeshi la JWTZ.
Amesema kuwa wamekuwa wakijifunza mafunzo mbalimbali
kutoka Israel ikiwemo mapambano dhidi ya ugaidi,uharamia,na vita vinavyoitwa
vya kisasa hivyo ni matumaini yao kuwa ziara hiyo itafungua milango ya
ushirikiano kati ya Tanzania na Israel.
Kwa upande wake waziri wa ulinzi wa Israel Azegdo
Lebaman amesema kuwa kwa sasa watatoa mafunzo ya ulinzi kwa kutumia tekinolojia
ya Tehama na namna ya kufanya uchunguzi katika matukio mbalimbali ya kiuhalifu.
TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA ISRAEL ILI KUIMARISHA JESHI LA ULINZI
Reviewed by safina radio
on
March 21, 2018
Rating:
No comments