WATANZANIA WATAKIWA KUFANYIA USAFI VINYWA VYAO


Ikiwa kesho ni maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa duniani jamii imetakiwa kufanyia usafi vinywa vyao ikiwa ni pamoja na kuhudhuria katika kiliniki za vinywa na meno ili kupima afya zao.



Image result for PICHA YA KINYWA CHWA MWANADAMU



Ushauri huo umetolewa na Dr Christian Maria ambaye ni mratibu wa afya ya kinywa  katika halmashauri ya Meru wakati akizungumza na Redio Safina kuhusu maadhimisho ya siku ya kinywa ambayo kitaifa itafanyika mkoani Mara.

Dr Maria amesema kuwa wananchi wengi wamekuwa wakisumbuliwa na matatizo ya kinywa kutokana na kutofanyia usafi vinywa vyao hivyo wanatakiwa kutumia dawa ya meno yenye floride ambayo inasaidia kuimaraisha meno na fizi.

Aidha amewataka wananchi kuhudhuria katika kiliniki za vinywa na meno ili kupima afya zao ili kama watabainika kuwa na matatizo waanze matibabu mapema na kupata ushauri.

Amesema kuwa katika kuadhimisha siku hiyo halmashauri ya wilaya ya Meru imejipanga kutoa huduma ya kinywa kwa watoto wapatao elfu kumi na sita mia tatu na kumi na nane  wenye mahitaji maalumu kutoka  katika  shule 60 za msingi za serikali kuanzia chekechea hadi darasa la tatu.

Hata hivyo kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya afya ya kinywa duniani kwa mwaka huu ni SEMA HA FIKIRIA KINYWA FIKIRIA AFYA.

WATANZANIA WATAKIWA KUFANYIA USAFI VINYWA VYAO WATANZANIA WATAKIWA KUFANYIA USAFI VINYWA VYAO Reviewed by safina radio on March 19, 2018 Rating: 5

No comments