8,592 YAELEZWA KUWA NI IDADI YA WAKIMBIZI WA ETHIOPIA KUINGIA KENYA.


NAIROBI.

Kamati ya msalaba mwekundu ya Kenya imetoa taarifa ikisema hadi sasa idadi ya wakimbizi wa Ethiopia waliokimbilia nchini humo imefikia elfu nane na miatano tisini na mbili tangu tarehe 10 mwezi huu, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka.

Image result for Kamati ya msalaba mwekundu ya Kenya
Taarifa hiyo imesema kuwa kamati ya msalaba mwekundu ya Kenya imewapatia wakimbizi hao chakula na huduma za afya, na wamepewa hifadhi katika wilaya ya Moyale ya kaunti ya Marsabit na eneo la Sololo karibu na mpaka wa nchi hizo mbili, kaskazini mwa Kenya.

Pia taarifa hiyo imesema vikosi vya Ethiopia viliwashambulia raia kwa makosa tarehe 10 mwezi huu kwenye eneo la Moyale lililoko karibu na mpaka kati ya Ethiopia na Kenya, na kusababisha vifo vya raia tisa na wengine 12 kujeruhiwa.

Kikosi hicho cha jeshi la Ethiopia kiliwashambulia raia hao wakidhani kuwa ni waasi wa kundi la upinzani Oromo Libertation Front hali iliyowasababisha baadhi ya raia wa Ethiopia kukimbilia nchini Kenya.
Hadi sasa kazi ya kuandikisha wakimbizi bado inaendelea.





8,592 YAELEZWA KUWA NI IDADI YA WAKIMBIZI WA ETHIOPIA KUINGIA KENYA. 8,592 YAELEZWA KUWA NI IDADI YA WAKIMBIZI WA ETHIOPIA KUINGIA KENYA. Reviewed by safina radio on March 15, 2018 Rating: 5

No comments