KAMWELWE AAGIZA MAMLAKA ZOTE ZA MAJI KULIPIA MAJI KWA MAMLAKA ZA MABONDE YA MAJI KAMA WANANCHI WANAVYOLIPIA MAJI WANAYOYATIBU.



Waziri wa Maji na Umwagiliaji Izack Kamwelwe ameziagiza Mamlaka zote za Maji Nchini kulipia maji wanayoyachukua katika Mamlaka ya Mabonde ya Maji hatua ambayo itachangia utunzaji wa vyanzo vya maji.

Image result for Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Izack Kamwelwe
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Izack Kamwelwe.
Waziri Kamwelwe ametoa agizo hilo mkoani Mbeya alipokuwa akizungumza na Wafanyakazi na Bodi ya Mamlaka ya Maji na Mazingira la jiji la Mbeya.

Aidha, Kamwelwe amezitaka mamlaka hizo kulipia maji wanayoyachukua kutoka vyanzo vya maji kwa kila mwezi kwa kuwa wananchi wanayalipia maji hayo wanayoyatibu, kwa ajili ya matumizi ya majumbani na viwandani.

Pia, amesema kuwa lazima Mamlaka hizo ziweze kushiriki katika kuchangia kutunza vyanzo vyanzo vya maji kutokana na kulipia maji hayo wanayochukua katika mabonde ya maji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Safu za Mazingira Mlima Mbeya Venance Awela pamoja na Afisa Maji Bonde la Ziwa Rukwa Grace Kitanda wamesema kuwa hali ya upatikanaji wa maji ni mzuri lakini wanakabiliwa na shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji.

Akiwa ziarani mjini Mbeya mbali na mambo mengine Waziri Mhandisi Kamwelwe ameweka jiwe la msingi katika ofisi mpya za Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mbeya.

KAMWELWE AAGIZA MAMLAKA ZOTE ZA MAJI KULIPIA MAJI KWA MAMLAKA ZA MABONDE YA MAJI KAMA WANANCHI WANAVYOLIPIA MAJI WANAYOYATIBU. KAMWELWE AAGIZA MAMLAKA ZOTE ZA MAJI KULIPIA MAJI KWA MAMLAKA ZA MABONDE YA MAJI KAMA WANANCHI WANAVYOLIPIA MAJI WANAYOYATIBU. Reviewed by safina radio on March 23, 2018 Rating: 5

No comments