WATU BINAFSI NA BAADHI YA TAASISI ZA URUSI ZAWEKEWA VIKWAZO NA MAREKANI.


Marekani imewawekea vikwazo watu binafsi na taasisi kadhaa za Urusi kwa tuhuma za kuingilia uchaguzi wa Marekani pamoja na mashambulizi ya mtandaoni.
Image result for Marekani
Alama muhmu za marekani.
Hata hivyo vikwazo hivyo havikuwagusa maafisa wa serikali ambao wapo karibu na Rais Vladimir Putin, na kusababisha wabunge wa pande zote mbili za vyama vikuu nchini Marekani kusema kwamba Rais Donald Trump anahitaji kuchukua hatua zaidi.
Wakati Marekani ikiwa chini ya shinikizo kubwa, hatua zilizotangazwa na Wizara ya Fedha ni za kwanza muhimu kuwahi kuchukuliwa dhidi ya nchi hiyo tokea Trump kuingia madarakani Januari 2017.
 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Ryabkov alisema kwamba Urusi inaandaa hatua za kulipiza kisasi, huku uhusiano kati ya nchi hizo mbili ukionekana kuharibika tena.





WATU BINAFSI NA BAADHI YA TAASISI ZA URUSI ZAWEKEWA VIKWAZO NA MAREKANI. WATU BINAFSI NA BAADHI YA TAASISI ZA URUSI ZAWEKEWA VIKWAZO NA MAREKANI. Reviewed by safina radio on March 16, 2018 Rating: 5

No comments