TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO TEHAMA YASAIDIA MAHAKAMA


Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Jaji Sekela Moshi amesema kuwa utaratibu wa kutumia Teknolokia ya Habari na Mawasiliano TEHAMA katika mahakama umesaidia kuweka takwimu za mwenendo wa kesi katika mahakama nyingi na hivyo kurahisisha utoaji wa hukumu.

Image result for picha ya jaji sekela moshi jaji wa mahakama kuu kanda ya arusha
JAJI SEKELA MOSHI.


Akifunga mafunzo kwa majaji sitini na moja kutoka kwa mahakama kuu kanda zote hapa nchini yaliyofanyika jijini Arusha Jaji Moshi amesema kuwa utaratibu wa kutumia TEHAMA katika kutoa hukumu umeonyesha matokeo chanya hasa katika mahakama ya biashara na vitengo vingine vya mahakama kuu jambo ambalo wataliendeleza.

Aidha, Jaji Moshi amesema kuwa takwimu za kimahakama kwa sasa ziko vizuri katika mfumo huo TEHAMA kutokana na kuwa unarahisisha katika upatikanaji wake kwa kuwa takwimu zisipopangiliwa vizuri inasababisha utoaji wa haki usiwe mzuri.

Kwa upande wake Jaji wa Mahakama Kuu na Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama ya Lushoto EJA ambacho kimetoa mafunzo hayo kwa ufadhili wa Benki Kuu ya Dunia Dk. Paul Kiwelu amesema kuwa watatoa mafunzo zaidi kwa majaji kwani bado kuna uhitaji mkubwa wa teknolojia hiyo.

TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO TEHAMA YASAIDIA MAHAKAMA TEKNOLOJIA YA HABARI NA MAWASILIANO TEHAMA YASAIDIA MAHAKAMA Reviewed by safina radio on March 29, 2018 Rating: 5

No comments