ZFDA YATEKETEZA KWA MOTO KILO 48 ZA NYAMA KUTOKA AFRIKA KUSINI.
ZANZIBAR.
Mamlaka ya Chakula na Dawa Zanzibar ZFDA imeteketeza
kwa moto kilo arobaini na nane za nyama kutoka Afrika Kusini zilizoingizwa
nchni kinyume cha sheria ambazo zinazosadikika kuwa na virusi vinavyo sababisha
ugonjwa wa MISTERIA.
Mkuu wa kitengo cha Uchambuzi wa hatari zinazotokana na Chakula kutoka Wakala wa Chakula na Dawa Zanzibar ZFDA Aisha Suleiman Akizungumza na Wandishi wa Habari. |
Mkuu wa Kitengo cha Utambuzi wa Hatari zinazotokana
na chakula wa ZFDA Aisha Suleiman amesema kuwa nyama hiyo iliyokuwa mali ya
Kampuni ya Kamar ya Vingunguti jijini Dar es salaam ilikamatwa katika Uwanja wa
ndege wa Kimataifa wa Amani Abeid Karume visiwani Zanzibar wiki iliyopita.
Aidha, amefafanua kuwa uamuzi wa kuteketezwa kwa
nyama hiyo ni kutokana na marufuku iliyopitishwa na Mamlaka hiyo ya uingizwaji
wa nyama, maziwa na samaki kutoka Afrika Kusini ambapo ugonjwa MISTERIA
umesababisha vifo vya watu mia moja themanini mpaka sasa.
Hivi karibuni Malmlaka ya Chakula na Dawa Zanzibar
imekabidhiwa cheti cha mfumo wa uhakiki ubora wa huduma cha kiwango cha
kimataifa cha IFO ikiwa ni kielelezo cha Mamlaka hiyo kusimamia misingi ya
ubora wa huduma katika kiwango cha kimataifa.
ZFDA YATEKETEZA KWA MOTO KILO 48 ZA NYAMA KUTOKA AFRIKA KUSINI.
Reviewed by safina radio
on
March 14, 2018
Rating:
No comments