TANZANIA YAAHIDI KUFANYA MAPITIO YA SERA ZAKE ZA NDANI ILI KULINDA MASOKO YA NDANI NA BIDHAA ZINAZOZALISHWA.
Serikali
imesema kuwa inaunga mkono makubalino ya kuundwa soko huru la pamoja barani Afrika ingawa itakuwa
makini katika kuangalia maeneo yaliyoanishwa kushirikiana ili kulinda maslahi
ya soko lake na bidhaa mbali mbali zinazozalishwa nchini.
Hayo
yamesemwa na Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa baada ya kutia saini
makubaliano ya kuanzishwa soko huru la pamoja katika mkutano wa Umoja wa Afrika
uliomalizika jana katika mji wa Kigali nchini Rwanda.
Aidha,
Mh. Majaliwa amesema kuwa mbali na kusainiwa makubaliano hayo kuna manufaa kwa serikali
hivyo inabidi kurudi nchini kukaa katika baraza la mawaziri kuungana na wanasheria ili kufanya mapitio kwa maeneo
ambayo Tanzania inaweza kupata makwazo kutokana na sheria zilizopo nchini.
Pia, amesema kuwa kuangalia
na mapitio hayo yatakayofanyika nchini yatasaidia katika kupata namna ya
kuendeleza uchumi kutoka uchumi wa chini hadi kufikia uchumi wa kati.
Hatua ya kusainiwa
makubaliano hayo ni ishiri ya kuleta matumaini kwa inchi za Afrika kuwa ndoto
ya waasisi wa Afrika katiika kushirikiana katika Nyanja za kiuchumi sasa inaelekea
kutimia licha ya kuwepo kwa baadhi ya mataifa kuomba muda wa kumalizia.
TANZANIA YAAHIDI KUFANYA MAPITIO YA SERA ZAKE ZA NDANI ILI KULINDA MASOKO YA NDANI NA BIDHAA ZINAZOZALISHWA.
Reviewed by safina radio
on
March 22, 2018
Rating:
No comments