KAMISHENI YA KISWAHILI YA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI YAKABILI NA CHANGAMOTO YA FEDHA


Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Kiswahili katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki Prof. Keneth Simala amesema Kamisheni ya Nchi hizo zinakabiliwa na changamoto ya rasilimali fedha katika majukumu yake ya kukuza lugha ya Kiswahili ambayo kwa sasa inazungumzwa na watu zaidi ya milioni 200 duniani.


Image result for PICHA YAKatibu Mtendaji wa Kamisheni ya Kiswahili katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki Prof. Keneth Simala



Prof. Simala ameyasema hayo katika mkutano wa wadau wa nchi wanachama pamoja na vyama vya kitaifa na kikanada vya kukuza lugha ya Kiswahili kilichofanyika jijini Arusha kujadili changamoto zinazowakabili.


Aidha, Prof. Simala amewaomba wananchi kushirki katika kutoa mawazo hususani wanaojihusisha na masuala ya Kiswahili katika tafiti zinazofanywa na kamisheni hiyo ili kufahamu changamoto na mahitaji yao.

Mmoja wa wadau wa lugha hiyo Kenny Waibora amesema kuwa katika kukuza Kiswahili inapaswa viongozi wanachama wa nchi hiyo kutumia lugha ya Kiswahili katika mikutano wanapoalikwa kuhutubia.

KAMISHENI YA KISWAHILI YA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI YAKABILI NA CHANGAMOTO YA FEDHA KAMISHENI YA KISWAHILI YA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI YAKABILI NA CHANGAMOTO YA FEDHA Reviewed by safina radio on March 27, 2018 Rating: 5

No comments