TRUMP AJIANDAA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA SEKTA YA TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO YA CHINA.


WASHINGTON.
Rais wa Marekani Donald Trump anajiandaa kuchukua hatua dhidi ya sekta ya tekinolojia na mawasiliano nchini China ikiwemo kuongezwa kwa viwango vya kodi kwa bidhaa zinavyoagizwa nchini humo.
Image result for Rais wa Marekani Donald Trump
Rais wa Marekani Donald Trump.
Wiki iliyopita maafisa wa ngazi ya juu wanaohusika na masuala ya biashara nchini humo waliwasilisha kwa Rais Trump mpango unaohusisha viwango vikubwa vya kodi.
Habari zinaeleza kuwa kiasi ya dola bilioni 30 zinatarajiwa kukusanywa kutokana na ushuru utakaotozwa kwa bidhaa zinazohusiana na sekta ya tekinolojia na mawasiliano zinazoingizwa nchini Marekani kutoka China.
Aidha, hatua hiyo inakuja wakati Marekani ikiyatuhumu makampuni ya kitekinolojia ya nchini China ambayo yamekuwa yakiyataka makampuni ya Marekani kutoa siri zake za kitekinolojia kabla ya kuruhusiwa kuendesha shughuli zao nchini humo.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa kamati inayohusika na masuala ya kodi katika baraza la wawakilishi, Kevin Brady amewaambia waandishi wa habari kuwa rais Trump amedhamiria kupambana dhidi ya tuhuma hizo za wizi wa kitekinolojia.

TRUMP AJIANDAA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA SEKTA YA TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO YA CHINA. TRUMP AJIANDAA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA SEKTA YA TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO YA CHINA. Reviewed by safina radio on March 14, 2018 Rating: 5

No comments