HALMASHAURI NA MIKOA ZATAKIWA KUTENGA FUNGU KWA AJILI YA KITENGO CHA HABARI, JAFFO.


ARUSHA.

Waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa  (TAMISEMI) Mh Suleman Jaffo ameagiza mikoa na halmashauri zote nchini kutenga fungu kwaajili ya kitengo cha habari ikiwa ni pamoja na  kuwaruhusu maafisa habari kuingia katika vikao vyote vya maamuzi ili waweza kutoa  habari sahihi kwa umma.

Image result for Mh Suleman Jaffo
Waziri wa nchi ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa  (TAMISEMI) Mh Suleman Jaffo.
Waziri Jafo ameyasema hayo mapema leo wakati akifunga kikao kazi cha 14 cha maafisa habari,mawasiliano na mahusiano serikalini  kilichomalizika leo mkoani Arusha.

Aidha Mh Jaffo amesema kuwa ipo mikoa na halmashauri ambazo haziwaruhushu maafisa habari kuingia katika vikao vya maamuzi kwa kukwepa baadhi ya taarifa kujulikana kwa umma ambapo waziri huyo amesema kuwa atahakikisha suala hilo linafanyiwa kazi ili kuondoa maswali mengi kwa wanachi dhidi ya majukumu yanayofanywa na serikali.

Waziri huyo pia mewataka wakuu wote wa idara na vitengo kuwapa takwimu sahihi maafisa habari ili waweze kuzitoa katika tovuti za halmashauri ili serikali pamoja na wananchi waweze kupata taarifa za maendeleo

HALMASHAURI NA MIKOA ZATAKIWA KUTENGA FUNGU KWA AJILI YA KITENGO CHA HABARI, JAFFO. HALMASHAURI NA MIKOA ZATAKIWA KUTENGA FUNGU KWA AJILI YA KITENGO CHA HABARI, JAFFO. Reviewed by safina radio on March 16, 2018 Rating: 5

No comments