UMOJA WA MATAIFA WAUNGA MKONO UCHAGUZI MPYA NCHINI ZIMBABWE


Umoja wa mataifa umetangaza kuunga mkono uchaguzi mpya unaoandaliwa kufanyika mwezi Julai nchini Zimbabwe na kuitaka serikali ya taifa hilo kutoa kipaumbele cha dharura kwa uchumi wa taifa hilo.

Image result for PICHA YA ACHIM STEINER AFISA UNDP
Achim Steiner 
Achim Steiner, kiongozi wa mpango wa maendeleo katika umoja wa mataifa UNDP alikuwa ziarani jijini Harare na kukutana na raisi Emmerson Mnangagwa.
Steiner amesema Umoja wa mataifa unaendelea kuunga mkono mchakato wa maandalizi ya uchaguzi na jitihada za kuinua uchumi.
Uchaguzi wa uraisi unatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi August ambapo Mnangagwa atakabiliwa na ushindani tangu alipochukua madaraka kutoka kwa aliyekuwa kiongozi mkongwe wa taifa hilo Robert Mugabe, ambaye alijiuzulu mwezi Novemba baada ya kutawala kwa takribani miongo minne.

UMOJA WA MATAIFA WAUNGA MKONO UCHAGUZI MPYA NCHINI ZIMBABWE UMOJA WA MATAIFA WAUNGA MKONO UCHAGUZI MPYA NCHINI ZIMBABWE Reviewed by safina radio on March 19, 2018 Rating: 5

No comments