Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Gabriel Mugabe amesema kuondoka kwake ofisini mwezi Novemba mwaka jana kulikuwa ni mapinduzi


Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Gabriel Mugabe amesema kuondoka kwake ofisini mwezi Novemba mwaka jana kulikuwa ni mapinduzi ya kijeshi na kutoa wito wa hali hiyo kubadilishwa.

Image result for PICHA YA MUGABE
RAIS MUGABE
Mugabe ametoa kauli hii kwenye mahojiano yake ya kwanza ya televisheni tangu ang’olewe madarakani na nafasi yake kuchukuliwa na rais wa sasa Emmerson Mnangagwa.
Aidha, Mugabe amesisitiza kuwa kilichofanyika ni mapinduzi ya kijeshi na kudai kuwa mrithi wake rais Mnangagwa asingeweza kuwa rais wa taifa hilo kama asingepata msaada wa jeshi.
Kauli ya Mugabe imekuja wakati huu wanaharakati kadhaa wakienda Mahakama ya Katiba kutaka kubatilishwa kwa namna rais Mnangagwa alivyoingia madarakani wakisema alitumia jeshi kupindua Serikali halali.

Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Gabriel Mugabe amesema kuondoka kwake ofisini mwezi Novemba mwaka jana kulikuwa ni mapinduzi Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Gabriel Mugabe amesema kuondoka kwake ofisini mwezi Novemba mwaka jana kulikuwa ni mapinduzi Reviewed by safina radio on March 16, 2018 Rating: 5

No comments