JESHI LA SAUDIA ARABIA LAANGUSHA MAKOMBORA SABA
Jeshi la anga la
Saudi Arabia limeyaangusha makombora saba yaliyofyatuliwa siku ya jumapili
kutoka Yemen na wapiganaji wa Kihouthi.
Kwa mujibu wa msemaji
wa muungano wa majeshi unaoongozwa na Saudi Arabia, Kanali Turki al-Malki, mtu
mmoja ameuawa baada ya kuangukiwa na mabaki ya makombora hayo, na wawili
wamejeruhiwa.
Taarifa ya Saudi Arabia
na washirika wake katika vita hivyo ambavyo vimedumu kwa miaka mitatu nchini
Yemen, imeeleza kuwa majeshi ya Saudi Arabia yaliyazuia makombora matatu
kaskazini mashariki mwa mji wa Riyadh, saa chache tu kabla ya usiku wa manane
wa kuamkia leo.
Aidha makombora
yaliyorushwa katika miji ya kusini mwa Najran, Jizan na Khamis Mushait pia
yaliharibiwa.
Shambulizi hilo ni la
tatu katika muda wa miezi mitano ambapo makombora yamerushwa mjini Riyadh huku
Wahouthi wakiimarisha hatua za kuonesha wanaweza kuushambulia mji mkuu wa Saudi
Arabia, hatua inayotishia kuzidisha uhasama katika kanda hiyo kati ya Iran na
Saudi Arabia.
JESHI LA SAUDIA ARABIA LAANGUSHA MAKOMBORA SABA
Reviewed by safina radio
on
March 26, 2018
Rating:
No comments