MKUU WA MKOA WA MANYARA ALEXANDER MNYETI AMEMUAGIZA MKURUGENZI WA WILAYA YA HANANG KUFUNGUA ZAHANATI YA KIJIJI CHA GANGAL
Mkuu wa Mkoa wa Manyara
Alexander Mnyeti amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
Brayceson Kibasa Kufungua Zahanati ya kijiji cha Gangal ndani ya mwezi mmoja ili
kuwaepushia wananchi adha ya kufuata huduma za afya kwa Umbali mrefu.
MKUU WA MKOA WA MANYARA ALEXANDER MNYETI |
Mnyeti ametoa agizo
hilo baada ya kusikia kero kubwa ya wananchi hao wanaokabiliwa na hadha
ya upatikanaji wa huduma za afya ambapo baadhi ya wagonjwa wanalazimika
kuzifuata huduma hizo katika hospitali ya Haydom iliyopo wilaya ya Mbulu.
Amesema nia ya Serikali
ni kuhakikisha kuwa wananchi wake wanazipata huduma muhimu kama za Afya kwa urahisi
na kwa wakati muafaka ili waweze kufanya shughuli zao za maendeleo wakiwa na
Afya njema
Ameongeza kuwa hakuna
sababu ya wananchi hawa kuendelea kuzifuata huduma za afya kilomita 23
kwasababu jengo hilo tayari limeshakamilika na amemtaka Mkurugenzi kupeleke
wahudumu wa afya ndani ya mwezi mmoja ili wananchi waweze kupata huduma bora za
afya.
Awali
akisoma taarifa ya ujenzi wa zahanati hiyo, mbele ya mkuu wa
mkoa huyo Alexander Mnyeti, Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt.Jackoracha Daimon amesema ujenzi wa zahanati kuwa ulianza mwaka 2013 kwa jitihada za wananchi kwa kuchangia fedha na nguvu kazi.
Dkt.Daimon alisema ujenzi wa zahanati hiyo umegharimu jumla ya
sh.ml,65,640,000 ambapo wananchi wamechangia sh mil. 26,000,000 huku halmashauri ya Wilaya hiyo ikiunga mkono jitihada za wananchi hao kwa kuchangia jumla ya sh.mil. 33, 640,000 kutoka mapato yake ya ndani.
mkoa huyo Alexander Mnyeti, Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt.Jackoracha Daimon amesema ujenzi wa zahanati kuwa ulianza mwaka 2013 kwa jitihada za wananchi kwa kuchangia fedha na nguvu kazi.
Dkt.Daimon alisema ujenzi wa zahanati hiyo umegharimu jumla ya
sh.ml,65,640,000 ambapo wananchi wamechangia sh mil. 26,000,000 huku halmashauri ya Wilaya hiyo ikiunga mkono jitihada za wananchi hao kwa kuchangia jumla ya sh.mil. 33, 640,000 kutoka mapato yake ya ndani.
MKUU WA MKOA WA MANYARA ALEXANDER MNYETI AMEMUAGIZA MKURUGENZI WA WILAYA YA HANANG KUFUNGUA ZAHANATI YA KIJIJI CHA GANGAL
Reviewed by safina radio
on
March 19, 2018
Rating:
No comments