SERIKALI INAKUSUDIA KULIWEZESHA SHIRIKA LA SIDO


Naibu waziri wa viwanda biashara na uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa serikali inakusudia kuliwezesha shirika la SIDO ili liweze kufanya kazi zake vizuri hapa nchini.
Image result for PICHA YA MHANDISI STELLA MANYANYA NAIBU WAZIRI WA VIWANDA
Naibu waziri wa viwanda biashara na uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya
Mhandisi Manyanya ameyasema hayo wakati Kamati ya kudumu ya bunge ya viwanda,biashara na mazingira kuitaka  serikali kuliwezesha kifedha shirika hilo mkoani Iringa ili kukuza sekta ya viwanda hapa nchini.
Wakizungumza baada ya kutembelea karakana ya SIDO ya mkoa wa Iringa wajumbe wa kamati hiyo wameonyesha kushangazwa na mashine zinazotumia tekinolojia za zamani na nyingine zikiwa hazifanyi kazi kutokana na uchakavu.
Meneja wa Sido wa mkoa wa Iringa Francesiko Saimon Amesema kuwa shirika hilo limeweza kutengeneza mashine mbalimbali za kukamua mafuta na kusaga nafaka.

SERIKALI INAKUSUDIA KULIWEZESHA SHIRIKA LA SIDO SERIKALI INAKUSUDIA KULIWEZESHA SHIRIKA LA SIDO Reviewed by safina radio on March 20, 2018 Rating: 5

No comments