SUMA-JKT YAKABIDHIWA KANDARASI YA KUJENGA MABANDA YA VIWANDA LA HEKARI TATU.


DODOMA.

Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage amemkabidhi mkandarasi SUMA-JKT eneo la hekari tatu mjini Dodoma kwa lengo la kujenga mabanda ya viwanda ili yawe mfano kwa wanaojifunza namna ya kuanzisha viwanda vyao.

Image result for Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage
Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage.

Katika Hafla ya Makabidhiano hapo jana Dk. Mwijage amesema ni fursa kwa wajasiriamali na wananchi wengine mkoani humo kuanzisha viwanda nchini chini ya usimamizi wa shirika la kusimamia na kuhudumia viwanda vidogodogo SIDO.

Aidha, amesema kuwa anawatafuta watu ambao hawana fedha wala hawafahamu lolote kuhusiana na viwanda ili kuwafundisha namna ya kupata fedha na kujenga viwanda huku akiwahitaji watu wenye fedha na hawafahamu namna ya kutumia fedha hizo waweze kujifunza matumizi mazuri ya fedha kwa uwekezaji wa viwanda.

Naye, Mkurugenzi wa SIDO Prof. Silvesta Mkunduji amesema kuwa shirika la SIDO limejipanga kuhakikisha kuwa azma ya serikali ya kufikia uchumi wa kati na wa viwanda unatekelezwa kwa vitendo, kwa kutoa elimu,teknolojia na mikopo kwa watanzania waliotayari kujiunga na SIDO.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa halmashauri ya Dodoma Mjini na Naibu Waziri wa ofisi ya waziri mkuu kazi ajira na watu wenye ulemavu Anthon Mavunde ameshukuru serikali kupitia wizara yake kujenga viwanda katika jimbo lake.

SUMA-JKT YAKABIDHIWA KANDARASI YA KUJENGA MABANDA YA VIWANDA LA HEKARI TATU. SUMA-JKT YAKABIDHIWA KANDARASI YA KUJENGA MABANDA YA VIWANDA LA HEKARI TATU. Reviewed by safina radio on March 15, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.