MLIPUKO WA BOMU WAUA WATU 11 NCHINI SYRIA.


Mlipuko wa bomu umewaua watu 11 katika jengo moja la ghorofa nne mjini Afrin, kaskazini mashariki mwa Syria, wakiwemo raia saba na wapiganaji wanne, muda mfupi baada ya Uturuki kutangaza kuukomboa mji huo kutoka kwa wapiganaji wa Kikurdi wa kundi la YPG.


Image result for PICHA YA MLIPUKO WA BOMU ULIOUWA WATU 11 NCHINI SYRIA USIKU WA KUAMKIA LEO


Bomu hilo ambalo linaelezwa kutegwa na magaidi, liliripuka wakati waasi wa kundi lijiitalo Jeshi Huru la Syria wakifanya msako baada ya kufanikiwa kuwaondoa wanamgambo wa Kikurdi na kutangaza udhibiti kamili, kufuatia wiki nane za mapambano makali.

 Wakati huo huo, Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema zaidi ya watu 6,000 wameondoka mashariki mwa mji uliozingirwa wa Ghouta.

Hilo linatokea baada ya Rais Bashir al Assad kufanya ziara katika eneo hilo linalowaaniwa kwa lengo la kuwapongeza wanajeshi kwa kufanikisha hatua ya kuwaonda waasi karibu na mji mkuu wa Damascus.

MLIPUKO WA BOMU WAUA WATU 11 NCHINI SYRIA. MLIPUKO WA BOMU WAUA WATU 11 NCHINI SYRIA. Reviewed by safina radio on March 19, 2018 Rating: 5

No comments