WATU 68 WAMEKUFA NCHINI VENEZUELA WALIPOJARIBU KUTOROKA JELA.


Watu 68 wamekufa nchini Venezuela wakati walipojaribu kutoroka kwenye jela moja baada ya moto kuzuka kwenye vyumba ambavyo walikuwa wakizuiliwa na Polisi.
Mwanasheria mkuu wa Serikali Tarel William ametoa idadi hiyo usiku wa kuamkia leo kwenye makao makuu ya polisi kaskazini mwa mji wa Carabobo, akilaumu kuwa moto huo uliwashwa kwa makusudi.
Kwa upande wake mkuu wa gereza hulo Carlos Nieto amesema baadhi ya wafungwa waliungua hadi kufa na wengine kwa kukosa hewa baada ya moto kuanza kuunguza magodoro na kuanza kuiba silaha kutoka kwa walinzi wakijaribu kutoroka.
Miongoni mwa waliokufa ni wanawake wawili ambao walienda kuwatembelea ndugu zao,na kutokana na tukio hilo waendesha mashtaka wanne wameteuliwa kuchunguza chanzo chake.
Picha zilizopigwa na vuguvugu la Nieto limeonesha askari wa zima moto wakijaribu kumuokoa mfungwa mmoja aliyekuwa akiungua.
Hata hivyo wafungwa wengi nchini Venezuela wanataabika kutokana na hali mbaya za magereza, kukosekana kwa mahitaji muhimu ya kibinadamu na jela kujaa kupita kiasi huku wakikabiliwa na hali mbaya ya kiuchumi.

WATU 68 WAMEKUFA NCHINI VENEZUELA WALIPOJARIBU KUTOROKA JELA. WATU 68 WAMEKUFA NCHINI VENEZUELA WALIPOJARIBU KUTOROKA JELA. Reviewed by safina radio on March 29, 2018 Rating: 5

No comments