NAIBU WAZIRI WA MALI ASILI NA UTALII MH. JAPHET HASUNGA AMESEMA SERIKALI ITAKAMILISHA UTARATIBU KUENDESHA JESHI LA USU.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mh Japhet
Hasunga amesema kuwa serikali ipo katika hatua za mwisho katika kukamilisha
utaratibu wote wa namna ya kuendesha jeshi Usu kwa Watendaji wake wa Idara ya
Maliasili kutoka mfumo wa zamani wa kiraia ambao utawawezesha watendaji kufanya
kazi kwa pamoja na kwa weledi.
NAIBU WAZIRI WA UTALII JAPHET HASUNGA |
Mh Hasunga ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo
ya kijeshi kwa Menejimenti, Mameneja wa Kanda na Maafisa Waandamizi wa wakala
wa huduma za misitu nchini ambapo amesema kuwa serikali ipo katika hatua za
mwisho katika kukamilisha utaratibu wote wa namna ya kuendesha jeshi hilo.
Aidha amesema kuwa kutokana na utaratibu ambao
wizara inayo kwa sasa ni kuhakikisha kuwa jeshi hilo litafanya kazi katika taasisi
zote za wizara ambazo zinahusika na uhifadhi wa malisili za taifa zikiwemo Mamlaka
ya Hifadhi Tanzani-TANAPA, Mamlaka ya Uhifadhi ya Ngorongoro-NGA.
Ameongeza kuwa utaratibu huo upo katika hatua za
mwisho za kukamilishwa baada ya rais kukubali kuanzishwa kwa vyeti
vilivyotayarishwa na wizara na hivyo jeshi hilo litaanzishwa mara moja.
Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu
Nchini Prof. Dosantos Silayo amesema kuwa mfumo huo utasaidia kuleta mabadiliko
katika utendaji.
NAIBU WAZIRI WA MALI ASILI NA UTALII MH. JAPHET HASUNGA AMESEMA SERIKALI ITAKAMILISHA UTARATIBU KUENDESHA JESHI LA USU.
Reviewed by safina radio
on
March 26, 2018
Rating:
No comments