UINGEREZA YATNGAZA KUFUKUZA WANADIPLOMASIA 23 WA URUSI.


LONDON.

Uingereza imetangaza leo kuwa itawafukuza kutoka nchini humo wanadiplomasia 23 wa Urusi na kusitisha mawasiliano ya ngazi ya juu na ikulu ya Kremlin, kuhusiana na shambulio la sumu ya kuua mishipa ya  fahamu dhidi ya jasusi wa zamani wa Urusi na binti yake nchini Uigereza.

Image result for Theresa May
Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May.

Waziri mkuu wa Uingereza Theresa May amelimbia bunge kuwa wana diplomasia hao 23, waliotambuliwa kuwa maafisa wa upelelezi ambao hawakubainishwa, wana muda wa wiki moja kuondoka nchini humo.

Mwaliko wa waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov pia umefutwa,huku Bi May akisema kuwa mawaziri wa Uingereza na wanafamilia ya Kifalme hawatahudhuria mashindano ya kombe la soka ya dunia yatakayofanyika nchini Urusi mwaka huu.

May ametangaza hatua hizo baada ya Urusi kupuuza muda wa mwisho ulitolewa kueleza namna sumu iliyotengenezwa na Umoja wa Kisovieti ilivyotumika dhidi ya Sergei na Yulia Skripal.

Ubalozi wa Urusi mjini London umelaani hatua hiyo ya May na kuitaja kuwa ya uhasama, isiyokubalika, na isiyo na mashiko.

UINGEREZA YATNGAZA KUFUKUZA WANADIPLOMASIA 23 WA URUSI. UINGEREZA YATNGAZA KUFUKUZA WANADIPLOMASIA 23 WA URUSI. Reviewed by safina radio on March 14, 2018 Rating: 5

No comments