Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassimu Majaliwa amesema nchi za Afrika ziunganishe nguvu.
Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassimu
Majaliwa amesema kuwa nchi za Afrika zinapaswa kuunganisha nguvu ili kupambana
na magonjwa yasiyoambukiza.
WAZIRI MKUU MAJALIWA |
Waziri mkuu ameyasema hayo jijini Dar-es-salaam wakati akifungua mkutano
wa 15 wa jumuiya ya mawaziri wa afya wa nchi za Afrika Mashariki,Kati na kusini
mkutano wenye lengo la kujadili mpango wa kuunganisha nguvu ili kuboresha sekta
ya afya.
Amesema kuwa pamoja na nchi hizo kupambana na magonjwa hayo bado kuna tatizo sugu la magonjwa ya
kifua kikuu,utapia mlo na magonjwa ya milipuko barani Afrika.
Kwa upande wake waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto
Mh Ummy Mwalimu amesema kuwa,Tanzania imejidhatiti kukabiliana na magonjwa hayo
kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya.
Naye katibu mkuu wa jumuiya hiyo Bw Yoshua Ndambisya amesema kuwa kuna
umuhimu wa kuwa na sera ya pamoja ili kuzuia magonjwa yasiyoambukiza .
Hata hivyo mkutano huo una mpango wa kujadili mpango wa kuunganisha nguvu
ili kuboresha sekta ya afya na kujadili
changamoto zinazokwamisha juhudi hizo.
Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kassimu Majaliwa amesema nchi za Afrika ziunganishe nguvu.
Reviewed by safina radio
on
March 20, 2018
Rating:
No comments