POLISI WAMKAMATA MTUHUMIWA MWENYE NUYARAKA MBALI MBALI ZA SERIKALI.
DAR-ES-SALAAM.
Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam linamshikilia
Bw Suleman Massudi kwa tuhuma za kukutwa na nyaraka mbali mbali za serikali ikiwemo
mihuri 53 ya kughushi, na vyeti feki vya chuo na taasisi za serikali.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam
Lazaro Mambosasa amesema kuwa mtuhumiwa huyo amekamatwa katika eneo la Yombo
Kilakala baada ya jeshi hilo kupata taarifa kuwa kuna kundi la watu linalijihusisha
na kutengeneza vyeti feki na mihuri.
|
Kamanda Mambosasa amesema kuwa miongoni mwa mihuri iliyokutwa
kwa mtuhumiwa huyo ni muhuri wa baraza la taifa la mitihani Tanzania, chuo cha
ufundi stadi VETA, Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Chuo cha Bandari, Chuo Kikuu
Huria, Chuo Kikuu Mtwara, Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Chuo cha Usafirishaji
NAT, Chuo cha usimamizi Fedha IAFM, pamoja na Chuo cha Uhasibu.
Katika hatua nyingine Kamanda Mambosasa amesema kuwa
wanawashikilia wanawake watatu kwa tuhuma za kutumia jina la rais mstaafu Dk.
Jakaya Mrisho Kikwete na familia yake kutapeli watu kwa kutumia mtandao wa
kijamii wa facebook.
POLISI WAMKAMATA MTUHUMIWA MWENYE NUYARAKA MBALI MBALI ZA SERIKALI.
Reviewed by safina radio
on
March 16, 2018
Rating:
No comments