MKUU WA WILAYA YA ARUSHA BW. FABIAN DAQQARO AMEWATAKA WAKAZI WA JIJI LA ARUSHA KUJITOKEZA KATIKA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI VITAMBULISHO VYA TAIFA.


Mkuu wa Wilaya ya Arusha Bw Fabian Daqqaro amewataka wakazi wa jiji la Arusha kujitokeza kwa wingi katika zoezi la uandikishwaji wa vitambulisho vya taifa pamoja na kutoa ushirikiano kwa NIDA ili kurahisisha zoezi hilo.


Image result for PICHA YA MKUU WA WILAYA YA ARUSHA FABIAN DAQQARO
Mkuu wa Wilaya ya Arusha Bw Fabian Daqqaro

Bw Daqqaro ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na  waandishi wa habari mkoani Arusha ambapo amesema kuwa zoezi la uandikishaji na upataji wa vitambulisho vya taifa litasaidia katika kupata idadi kamili kwenye matumizi ya masuala ya serikali pamoja na kuimarisha daftari la wapiga kura.

Aidha amesema kuwa zoezi la NIDA katika Wilaya ya Arusha limeshafanyika kwenye kata zaidi 15 ambapo kwa sasa zoezi hilo lipo katika kata ya kati,ofisi za NIDA na ofisi za Mkuu wa Mkoa pamoja na kata ya Muriett maeneo ya Mkonoo,Morombo na Nadosoito.

Vilevile ameeleza kuwa zoezi hilo ni la muhimu kwa ajili ya maendeleo ya nchi katika Nyanja mbalimbali ikiwemo za kiuchumi,kisiasa na kijamii pamoja na kupata takwimu sahihi  katika kutengeneza mipango mbalimbali ya kimaendeleo.

Hata hivyo amesema kuwa mpaka sasa tayari wamewasambaza maafisa uhamiaji kwa kila kituo ambacho zoezi la uandikishaji linafanyika kwa lengo la kugundua na kukamata wahamiaji haramu.

MKUU WA WILAYA YA ARUSHA BW. FABIAN DAQQARO AMEWATAKA WAKAZI WA JIJI LA ARUSHA KUJITOKEZA KATIKA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI VITAMBULISHO VYA TAIFA. MKUU WA WILAYA YA ARUSHA BW. FABIAN DAQQARO  AMEWATAKA WAKAZI WA JIJI LA ARUSHA KUJITOKEZA KATIKA ZOEZI LA UANDIKISHWAJI VITAMBULISHO VYA TAIFA. Reviewed by safina radio on March 16, 2018 Rating: 5

No comments