WANANCHI WA MISRI WANAPIGA KURA LEO KUMCHAGUA RAIS
Wananchi wa Misri wanapiga kura leo kuchagua rais kati ya rais
wa sasa Abdel Fattah al-Sisi na mgombea mwingine mdogo ambaye anakabiliwa na
ukosoaji mkubwa kuwa ni kibaraka wa Sisi.
RAIS WA SASA WA MISRI ABDEL FATTAH AL -SISI |
Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa majira ya saa moja asubuhi katika zoezi litakalochukua siku
tatu ambapo rais al-Sisi anatarajiwa kushinda kwa muhula wa pili wa kipindi cha
miaka minne.
Usalama umeimarishwa nchi nzima kutokana na tishio la
kutekelezwa mashambulizi na wapiganaji wa kiislamu wa Islamic State ambao
wametishia kushambulia maeneo ya mitambo ya kupokelea matokeo na hata kwenye
vituo.
Siku ya Jumamosi polisi wawili waliuawa katika shambulio la bomu
kwa kutumia gari, shambulio likilenga msafara wa mkuu wa usalama kwenye jimbo
la Alexandria.
Jumla ya wapiga kura milioni 60 wameandikishwa kupiga kura
katika taifa ambalo asilimia kubwa raia wake ni waarabu.
WANANCHI WA MISRI WANAPIGA KURA LEO KUMCHAGUA RAIS
Reviewed by safina radio
on
March 26, 2018
Rating:
No comments