RAIS WA ZAMANI WA UFARANSA NICOLAS SARKOZY AHOJIWA KWA MARA YA PILI.
Rais wa zamani wa
Ufaransa Nicolas sarkozy amerejea katika kituo cha polisi leo ili kuhojiwa kwa
mara ya pili kuhusiana na madai kwamba kiongozi wa zamani wa Libya Muamar
Gaddafi alimsaidia kwa fedha katika kampeni yake ya uchaguzi wa rais mwaka
2007.
RAIS WA ZAMANI WA UFARANSA NICOLAS SARKOZY |
Sarkozy mwenye umri
wa miaka 63, aliwasili katika ofisi za maafisa wanaohusika na rushwa,
utakatishaji fedha na ukwepaji kodi magharibi mwa mji wa Paris katika kitongoji
cha Nanterre.
Rais huyo alikamatwa
kwa mara ya kwanza jana asubuhi, lakini aliondoka kutoka katika jengo hilo la
polisi usiku wa manane. Mawakili wake hawakujibu walipotakiwa kutoa maelezo.
Tangu mwaka 2013,
majaji waliokuwa wanafanya uchunguzi wamekuwa wakichunguza ripoti za vyombo vya
habari, pamoja na taarifa za mtoto wa gaddafi Seif al-Islam, ambazo zinadai
kwamba fedha zilitolewa katika juhudi za Sarkozy kugombea urais.
RAIS WA ZAMANI WA UFARANSA NICOLAS SARKOZY AHOJIWA KWA MARA YA PILI.
Reviewed by safina radio
on
March 21, 2018
Rating:
No comments