WAUZA MADAWA YA KULEVYA 13 WAUAWA NA JESHI LA POLISI UFILIPINO.
Jeshi
la Polisi nchini Ufilipino limewaua washukiwa 13 wa biashara haramu ya madawa ya
kulevya katika operesheni iliyoendeshwa katika mkoa wa Bulacan nchini
humo.
Jeshi hilo limefahamisha kuwa limeshambuliwa na
walanguzi hao wa madawa ya kulenvya na polisi kujihami na kisha kufyatua risasi
nakufanikiwa kuwaua washukiwa hao 13.
Katika tukio hilo zaidi ya watu 100 wanaoshukiwa
kuhusika na biashara haramu ya madawa ya kulevya wamekamatwa.
Watu zaidi ya elfu nne wamekwisha kuuawa nchini
Ufilipino wakishukiwa kuhusika na baishara ya madawa ya kulevya tangu rais
Rodrigo Duterte kuchaguliwa kuwa rais wa Ufilipino.
Mashirika ya kutetea haki za binadamu yanailaumu
serikali ya Duterte yakidai kuwa inakiuka haki za binadamu.
WAUZA MADAWA YA KULEVYA 13 WAUAWA NA JESHI LA POLISI UFILIPINO.
Reviewed by safina radio
on
March 23, 2018
Rating:

No comments