RAIS MAGUFULI AMESEMA KUWA SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA SEKTA YA AFYA NCHINI.


Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John Magufuli amesema kuwa serikali itaendelea kuboresha sekta ya afya kwa kuongeza bajeti ili kuhakikisha kuwa wananchi wake wanapata huduma nzuri za afya.

Image result for picha ya rais magufuli
RAIS MAGUFULI

Rais Magufuli ameyasema hayo  leo jijini Dar-es-salaam wakati akizindua magari 181 ya kusambaza vifaa tiba katika maeneo mbalimbali hapa nchini ambayo yametolewa na shirika la kimataifa la Global Fund.

Amesema kuwa watanzania wasipokuwa na afya njema hawataweza kufanya kazi hasa kipindi hiki serikali inapohimiza uchumi wa viwanda hivyo wameona ni vyema wakawekeza kwenye sekta ya afya,ambapo pia amelishukuru shirika hilo kwa kutoa msaada huo wa magari ambayo yatarahisisha usambazaji wa dawa katika hospitali na vituo mbalimbali vya afya hapa nchini.

Kwa upande wake waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Ummy Mwalimu amesema kuwa serikali ya awamu ya tano inaendelea kuboresha miundombinu mbalimbali ya afya ikiwemo vituo vya afya katika mikoa ya Geita,Kagera,Mwanza,Tanga,Simiyu,Tabora na Singida.

Naye mkurugenzi mkuu wa bohari kuu ya dawa(MSD) Bw Lauran Bwanakunu amesema kuwa mgari hayo yaliyozinduliwa yatasaidia kuongeza uwezo wa kusambaza vifaa tiba hadi kwenye vituo vya afya tofauti na hapo awali ambapo usambazaji wa dawa ulikuwa unaishia hospitali za wilaya.

RAIS MAGUFULI AMESEMA KUWA SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA SEKTA YA AFYA NCHINI. RAIS MAGUFULI AMESEMA KUWA SERIKALI ITAENDELEA  KUBORESHA SEKTA YA AFYA NCHINI. Reviewed by safina radio on March 26, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.