HUDUMA YA REDIO SAFINA KESHO IMEANDAA MAOMBI MAALUMU YA KUHITIMISHA KITENDO CHA KIMAANI CHA KUCHOVYA MIGUU KWENYE MAFUTA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KWENYE VIFUNGO VYA MUDA MREFU.


Imebainishwa kuwa watu wengi wamepigwa na shetani katika maeneo mbalimbali ikiwemo elimu,uchumi,afya pamoja na karama na vipawa baada ya watu hao kubainika kuwa ni malango ya mafanikio katika familia zao.

Image result for radio safina

Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana imekuandalia maombi maalumu ya hitimisho la kuchovya miguu kwenye mafuta kwa ajili ya kufunguliwa kwenye vifungo vya muda mrefu.

Aidha kesho katika ukumbi huo kutafanyika maombi ya ukombozi kwa wazaliwa wa kwanza kama lango kwani wengi wameshambuliwa na adui pindi wanapo jaribu kutoa msaada kwa ndugu zao kama vile kuwasomesha,kuwapatia huduma za matibabu,chakula na malazi au kusuluhisha migogoro ya kifamilia.

Vile vile kwa mujibu wa somo hilo malango ya mzaliwa wa kwanza yanaposhughulikiwa au kukamatwa na adui mtu huyo hushindwa kufanya jambo lolote la kimaendeleo katika maisha yake kutokana na shetani kuondoa kibali cha mzaliwa huyo wa kwanza mbele ya ndugu zake pamoja na jamii kwa ujumla.

Hata hivyo siku ya kesho kila mmoja anakumbushwa kubeba mafuta yaliykuwa yakiombewa na watumishi wa Mungu kwa njia ya redio ili kufanya kitendo cha imani cha kushughulikia na kufunguliwa malango ya mzaliwa wa kwanza.


HUDUMA YA REDIO SAFINA KESHO IMEANDAA MAOMBI MAALUMU YA KUHITIMISHA KITENDO CHA KIMAANI CHA KUCHOVYA MIGUU KWENYE MAFUTA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KWENYE VIFUNGO VYA MUDA MREFU. HUDUMA YA REDIO SAFINA KESHO IMEANDAA MAOMBI MAALUMU YA KUHITIMISHA KITENDO CHA KIMAANI CHA KUCHOVYA MIGUU KWENYE MAFUTA KWA AJILI YA KUFUNGULIWA KWENYE VIFUNGO VYA MUDA MREFU. Reviewed by safina radio on March 23, 2018 Rating: 5

No comments