MNADHIMU MKUU WA JESHI LA ULINZI LUTENI JENERALI YAKUB MOHAMED AMEWATAKA MAAFISA NA ASKARI WA JWTZ KUMPA USHIRIKIANO.
Mnadhimu mkuu wa jeshi la ulinzi la wananchi wa
Tanzania Luteni Jenerali Yakub Mohamed amewataka maafisa na askari wa JWTZ
kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake.
Luten Jenerali Mohamed ametoa kauli hiyo katika
ziara yake ya kwanza ya kutembelea jeshi la Kigoma kwa lengo la kujitambulisha
na kubaini changamoto mbalimbali zinazowakabili katika masuala ya ulinzi na
usalama.
Hata hivyo Jenerali huyo amefanya ziara hiyo ya
kwanza mkoani Kigoma baada ya kuteuliwa hivi karibuni na rais wa jamuhuri ya
muungano wa Tanzania Mh John Magufuli kuwa mnadhimu mkuu wa jeshi la wananchi Tanzania.
MNADHIMU MKUU WA JESHI LA ULINZI LUTENI JENERALI YAKUB MOHAMED AMEWATAKA MAAFISA NA ASKARI WA JWTZ KUMPA USHIRIKIANO.
Reviewed by safina radio
on
March 15, 2018
Rating:
No comments