KOREA KASKAZINI IKO TAYARI KUACHANA NA MPANGO WAKE WA SILAHA ZA NYUKLIA.
Kiongozi wa Korea
Kaskazini, Kim Jong Un amemwambia Rais wa China Xi Jinping kwamba utawala wake
uko tayari kuachana na matumizi ya silaha za nyuklia.
RAIS WA KOREA KASKAZINI KIM JONG UN |
Shirika la habari la China, Xinhua limeripoti
hayo leo, wakati ambapo Kim, ambaye ni mshirika wa China amefanya ziara yake ya
kwanza nje ya nchi, kabla mikutano ya kilele na Korea Kusini na Marekani.
Kim amesema suala la kuachana na silaha za
nyuklia katika Rasi ya Korea linaweza kutatuliwa, kama Korea Kusini na Marekani
zitaitikia juhudi zao kwa nia njema, kuweka mazingira ya amani na utulivu, huku
wakichukua hatua zaidi kwa ajili ya kupatikana kwa amani.
Wakati huo huo,
Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe amesema nchi yake inataka kupata maelezo ya
kina kutoka kwa China, kuhusu mazungumzo yaliyofanyika kati ya Xi Jinping na
Kim.
KOREA KASKAZINI IKO TAYARI KUACHANA NA MPANGO WAKE WA SILAHA ZA NYUKLIA.
Reviewed by safina radio
on
March 28, 2018
Rating:
No comments